Jiunge kupata chapisho jipya kwa barua pepe!

jua'hatutumi spam!.

Jumanne, 7 Mei 2013

TEKNOLOGIA YA GPRS



Mambo yamebadilika sana kwenye suala la matumizi ya simu za mikononi! Vitu ambavyo vilidhaniwa visingewezwa kufanywa kwa kutumia simu za mikononi  vinafanyika sasa, tena kwa kubonyeza kifungo/batanicha keypad tu! Teknologia mbalimbali zimevumbuliwa zinazoruhusu kutumia simu kwa kutuma data kwa kasi kubwa!, Ndio, data za barua-pepe, za kuperuzi tovuti na matumizi mengine ya kisasa ya simu za mikononi!. Yote haya yamewezekana kwa kutumia teknologia ya GPRS! kirefu chake ni General Packet Radio Service. Teknologia hii inatumika kwenye kizazi cha pili cha simu za selula/rununu (2G mobile phones) kuzisaidia kupokea an kutuma data kwa kasi kubwa!. GPRS inaruhusu simu kuunganishwa muda wote kwenye mtandao, hivyo kama umetumiwa MMS (MulitiMedia Services), itapakuliwa kwenye simu yako na kutaarifiwa kuwa una MMS mpya, hivyo huna haja ya kuipakua unahitajika kubonyeza tu batani kuisoma! Teknologia hii inaweza kutoa kasi ya 32kbps mpaka 48kbps. Sifa nyingine kuu ya teknologia hii ni uwezo wake wa kuruhusu utumaji na upokeaji wa data hata wakati unaongea na simu! Matumizi ya GPRS huchajiwa kwa kiwango cha data ulizotumia, sio kwa muda uliotumia kama ilivyo kwa matumizi ya kawaida ya huduma ya sauti ya simu. Hii teknologia imeziwezesha simu zinazoitumia kuwa na ufanisi unaokaribia kidogo na ule wa zile zinazotumia teknologia ya kizazi cha tatu (3G mobile technology)!, ila tofauti kubwa ya 3G ni uwezo wake wa kuwa na kasi kubwa ya kutuma na kupokea data. Teknologia ya GPRS iliyoboreshwa inaweza kusapoti huduma mbalimbali kama kuperuzi mtandao, kutuma barua-pepe, na ujumbe wa picha, sauti na video(MMS), hivyo teknologia hii yaweza itwa pia 2.5G!

Mchoro unaonyesha namna teknologia ya GPRS inavyoshirikiana na teknologia nyingine kufanikisha mawasiliano ya data



soma zaidi  maelezo ya GPRS

Socializer Widget By Blogger Yard
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →

0 comments:

Chapisha Maoni